Ni msimu mwingine wa Soko la Wazi la Mkulima Market maarufu kama Mkulima Soko. Tunakukaribisha kuungana na wazalishaji na wachakataji bidhaa mbalimbali za kilimo, ufugaji, uvuvi na uwindaji kuona wazalishaji kutoka kila pembe ya Tanzania. 
Katika Mkulima Soko utapata fursa ya kuona, kupata elimu na kununua bidhaa bora zinazozalishwa Tanzania. 
Soko hili la Wazi litafanyika kuanzia tarehe 30 Agosti hadi 2 Septemba 2017 (Jumatano, Alhamisi, Ijumaa na Jumamosi). Karibu ujifunze ufugaji wa sungura, samaki na nyuki. Kama kawaida soko litafanyika kwenye Maegesho ya Magari ya Research Flats, mbele ya Jengo la Ndaki ya Kilimo na Teknolojia za Uvuvi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Msimu huu kutakuwa na wazalishaji wapatao 60 watakaoleta bidhaa mbalimbali fresh na zilizochalatwa. 

Katika soko hili kutakuwa na mambo makubwa manne na ili kuyajua mambo hayo manne .... BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...