Tarehe 09.08.2017 majira ya saa 21:00 Hrs (saa tatu usiku) katika mapori ya kijiji cha Rungungu mtuhumiwa akiambatana na Askari Polisi alikwenda kuonyesha Ngome ya watuhumiwa wenzake aliokuwa anashirikiana nao kufanya uhalifu.
Baada ya kukaribia eneo la tukio ulitokea upinzani mkali wa majibizano ya risasi jambo lililopelekea hata Abdallah Abdallah Mbindimbi @Abajani kujeruhiwa na risasi sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kufuatia majibizano hayo, Askari Polisi walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu 12 (kumi na mbili.
Jitihada zilifanyika kuwapeleka Hospitali majeruhi wote 13 (kumi na tatu) ingawa baadae walifariki dunia kwa nyakati tofauti wakipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na kuvuja damu nyingi zilizosababishwa na majereha ya risasi sehemu mbalimbali za miili yao.
Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es salaam.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akipata maelezo kutoka kwa
Mkuu wa Operesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi
(DCP) Liberatus Sabas kuhusiana na tukio la kuuawa wahalifu 13 katika
majibizano ya risasi baina ya Polisi na wahalifu hao katika eneo la
Tangibovu, Kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafa ya Kibiti. Chini
ni silaha 8 aina ya SMG pamoja na vifaa vingine zilizopatikana katika
majibizano hayo. – Picha na Jeshi La Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akionesha makasha ya
risasi (magazine) ambazo ni miongoni mwa makasha 8 yaliyokuwa
yakitumiwa na wahalifu katika eneo la Tangibovu, Kijiji cha Miwaleni
Kata ya Mchukwi, Tarafa ya Kibiti. Wa kwanza kushoto ni Kamishina wa
Polisi Jamii (CP) Mussa Alli Musa akifuatiwa na Mkuu wa Operesheni
Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus
Sabas. Katika tukio hilo Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwaua wahalifu 13
ambao walikuwa wakifanya mauaji Kibiti. – Picha na Jeshi La Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akielezea baadhi ya vitu
mbalimbali vilivyokuwa vikitumiwa na wahalifu 13 waliouawa katika eneo
la Tangibovu, Kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafa ya Kibiti
ambapo jumla ya silaha 8 aina ya SMG, risasi 158, pikipiki 2, pamoja
na begi la nguo vilivyokuwa vikitumiwa na wahalifu hao. Kushoto ni
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai (CP) Robert Boaz.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akionesha silaha aina ya
SMG ambayo ni miongoni mwa silaha 8 zilizokuwa zikitumiwa na wahalifu
13 waliouawa katika majibizano ya risasi baina yao na Jeshi la Polisi
katika eneo la Tangibovu, Kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafa
ya Kibiti. Wa kwanza kulia ni Kamishina wa Polisi Jamii (CP) Mussa Alli
Musa akifuatiwa na Mkuu wa Operesheni Maalumu za Jeshi la Polisi,
Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus Sabas. – Picha na Jeshi La
Polisi.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akiongea na wananchi wa
Kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafa ya Kibiti alipokuwa akitoka
kukagua eneo la tukio walipouawa wahalifu 13 katika majibizano ya
risasi baina yao na Jeshi la Polisi katika eneo la Tangibovu.
(Picha na Jeshi La Polisi.)
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
(Picha na Jeshi La Polisi.)
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...