Asteria Muhozya na Zuena Msuya, DSM
Serikali imesema kuwa ifikapo tarehe 30 Agosti, mwaka huu itatangaza Zabuni ya kuanza ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme wa kiasi cha megawati 2,100 katika Maporomoko ya Maji ya Mto Rufiji. (Stiegler’s Gorge).
Hayo yalielezwa jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani wakati akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Dkt. Kalemani alitoa wito kwa Watanzania, Taasisi Binafsi na Kampuni zenye uwezo kutoka ndani na nje ya nchi kujitokeza kuomba zabuni hiyo mara baada ya kutangazwa na kuongeza kuwa, Serikali inazo fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi husika.
Aliongeza kuwa, tayari taratibu za awali za utekelezaji wa mradi huo zimekwisha anza ambapo Wataalam kutoka ndani na nje ya nchi wamekwishakutana na kupitia nyaraka za mradi ikiwemo kuchagua eneo ambalo mradi husika utajengwa.
 Watalaam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wakielendelea na kazi ya kukamilisha nyaraka mbalimbali kuhusu mradi husika.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kutangazwa Zabuni ya Mradi wa Kuzalisha umeme wa Rufiji. Wanaofuatilia ni Wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...