Mwenyekiti wa New Life In Christ Mkoani Kilimanjaro, Bi. Elly Makyao (kulia) akikabidhi misaada ya kibinadamu ya Wafungwa waliopo Magerezani nchini kwa Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa. Hafla fupi ya Makabidhiano ya Misaada hiyo imefanyika leo Septemba 08, 2017 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga – Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa akitoa hotuba fupi wakati wa hafla ya kupokea misaada ya kibinadamu kwa Wafungwa waliopo Magerezani iliyotolewa na Asasi ya "New Life In Christ" leo Septemba 08, 2017 katika Viwanja vya Gereza Kuu Karanga - Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akiwakabidhi cheti cha shukrani Viongozi wa Asasi ya "New Life In Christ" kwa kutambua mchango wao kwa niaba ya Jeshi la Magereza Tanzania na Serikali kwa ujumla.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akimsukuma askari ambaye ameketi kwenye Baiskeli Maalum ya kubebea wagonjwa wasiojiweza ambayo ni miogoni mwa vifaa mbalimbali vilivyotolewa kama msaada kwa Jeshi la Magereza na Asasi ya "New Life In Christ"(kushoto) ni Mkurugenzi wa Doricas Aide International anayeshughulikia Miradi ya Afya katika nchi za Africa, Bi. Mirjam Verwij.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...