Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inapenda kuwajulisha wazee wote wa mkoa wa Dar-es-salaam Wilaya ya Ubungo kuwa zoezi la Usajili na Utambuzi lenye lengo la kuwapatia Vitambulisho vya Taifa linaendelea sambamba na zoezi la Usajili wa Kadi za Bima ya Afya kwa wazee chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. 
Wahusika ni wazee wote wanaoishi Wilaya ya Ubungo. Unachotakiwa kufanya ni kuchukua na kujaza fomu ya maombi ya  Usajili. Fomu zinapatikana ofisi ya Mtaa unakoishi au Ofisi ya Kata. Unapojaza fomu ya maombi unatakiwa kuweka na nakala ya  viambatisho muhimu vinavyokutambulisha vile ulivyonavyo mathalani Kadi ya Kupigia kura, Barua ya Serikali ya Mtaa, vyeti vya shule na kisha fika na fomu yako ikiwa imejazwa pamoja na vivuli (photocopy) ya viambatisho hivyo kwenye kituo cha karibu kusajiliwa. 
Unapofika kusajiliwa unashauriwa kwa ajili ya ubora wa picha kutovaa nguo nyeupe, kijivu, bluu, pinki, au rangi yoyote inayoshabihiana na nyeupe, nguo zenye nembo, kofia aina yeyote ama kupaka hina kwenye viganja vya mikononi. 
Kwa kuanza wiki ijayo Ratiba ya Usajili itakuwa ni kama ifuatavyo:-

Na
KITUO CHA USAJILI
MUDA
TAREHE
1.
Kata ya  Makurumla

Saa 3:00 – 11:00 jioni
11/09/2017
2.
Kata ya Manzese

Saa 3:00 – 11:00 jioni
12/09/2017
3.
Kata ya Sinza
Saa 3:00 – 11:00 jioni
13/09/2017
4.
Kata ya Makuburi
Saa 3:00 – 11:00 jioni
14/09/2017

Utaratibu wa Usajili katika Kata zingine tutaendelea kuwafahamisha. Kupata maelezo zaidi tafadhali wasiliana na mtendaji wako wa Mtaa au Mtendaji Kata. 
Kwa taarifa zaidi kuhusu Vitambulisho vya Taifa tembelea Tovuti yetu www.nida.go.tz au ukurasa wetu wa facebook -nidatanzania au twitter @nidatanzania 
Wazee jitokezeni kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa ili mtambulike na kupata huduma za kijamii kwa haraka na kwa uhakika zaidi.


Limetolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...