Katika kuboresha huduma za kibenki nchini Maendeleo Bank lao imetoa zawadi kwa washinidi wake wanne wa droo ya kwanza ya bahati nasibu ya ‘Maendeleo pamoja na wewe’ iliyochezeshwa tarehe 31/8/2017 Jijini Dar es salaamHafla ya kuwapatia washindi hao zawadi ilifanyika leo katika ukumbbi wa ‘Mviringo hall’ uliopo makao makuu ya Benki hiyo ‘Luther House’ posta Jijini hapa ambapo washindi hao wanne walijishindia zawadi tofauti tofauti ikiwemo Ada za shule, tani za Saluji,Mabati pamoja na kiwanja, 
Akizungumza katika hafla hiyo fupi mkuu wa kitengo cha biashara Maendeleo Bank Peter Tarimo amesema katika kuhakikisha Maendeleo Bank inakuwa karibu na wateja wao imeamua kuwahamasisha hasa wazazi kufungua Account za Benki kwa ajili ya watoto wao ili kuweza kuwajengea utamaduni wa kuhifadhi fedha
“Mtakumbuka kuwa kampeni hii ilizinduliwa mwanzoni mwa mwezi wa nane na wateja wengi walishiriki, Droo ilichezeshwa chini ya usimamizi wa bodi ya michezo ya kubahatisha (Gaming Board) na kuwapata washindi hawa wanne ambao leo tunakwenda kuwakabidhi zawadi zao” 
Aidha tarimo aliongeza kuwa Droo ya pili ya bahati na sibu hiyo inatarajiwa kuchezeshwa mwezi wa Novemba mwaka huu na ya tatu itakuwa mwezi Disemba ili kupisha zoezi la uuzaji wa Hisa litakaloanza tarehe 18/9/2017 na kutarajiwa kumalizika mwezi October 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...