Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala akisalimiana na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala kabla ya kuanza kwa mkutano wa watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Washiriki wa mkutano huo wakianza kwa kumtanguliza Mungu kwanza.
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa akisoma hotuba ya Kamishna Mkuu wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa makamshina na watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (kushoto) akibadilishana mawazo na baadhi ya watendaji waandamizi wa mamlaka hiyo wakati wa mapumziko ya Mkutano wa Mamlaka za mapato za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofunguliwa jijini Dar es Salaam leo Septemba 27 2017. Kutokea (kushoto) ni Kaimu Naibu Kamishna wa Upelelezi wa Kodi, Salim Kessi, Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...