Marehemu Mama Philberta Mapunda, mke wa aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali (Tanzania Standard Newspapers – TSN), Mzee Joseph Mapunda, amezikwa leo jioni Septemba 14, 2017 katika makaburi ya Luguluni, Kwembe, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam,
Marehemu Mama Mapunda, aliyefariki dunia usiku wa Septemba 11, 2017 jijini Dar es salaam, alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya moyo na shinikizo la damu. Alikuwa na umri wa miaka 62.
Mume wa Marehemu, Mzee Mapunda, pia ni mjumbe wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Uongozi wa Michuzi Media Group na wafanyakazi wote wanatoa pole kwa familia ya Mzee Mapunda na kuwatakia uvumilivu katika wakati huu mgumu.
Mola na aiweke roho ya marehemu mahala pema Peponi – Amina.
Marehemu Mama Philberta Mapunda, mke wa aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali (Tanzania Standard Newspapers – TSN), Mzee Joseph Mapunda, ukiwasili nyumbani  kabla ya kwenda mazishini

Ibada  ya mazishi ya Marehemu Mama Philberta Mapunda

Aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali (Tanzania Standard Newspapers – TSN), Mzee Joseph Mapunda, akiweka shada la maua juu ya kaburi la mkewe Mama Philberta Mapunda wakati wa mazishi katika makaburi ya Luguluni, Kwembe, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...