Mwenyekiti wa Bodi TanTrade Eng. Christopher Chiza akiongea na Waandishi wa Habari katika Mpaka wa Mabamba Wilayani Kibondo, Kigoma baada ya kumaliza ziara ya siku nne ya kutembelea Mipaka mitano ya Tanzania na Burundi iliyopo Mkoani Kigoma.
Lengo la ziara hii lilikuwa la kukutana na Taasisi za Serikali na Wafanyabiashara kujadili mpango wa kuwekeza miundombinu ya kurasimisha biashara ya Mpakani na kuhamasisha ushiriki katika Kongamano na Maonesho ya Tanzania Bujumbura Burundi yatakayofanyika kuanzia tarehe 27.09 mpaka tarehe 1.10.2017. Karibuni sana tushiriki katika matukio haya ya muhimu ya kihistoria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...