Na Tiganya Vincent- RS-Tabora

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imeawaagiza Maafisa Ugani kuanza mapema maandalizi ya kilimo cha pamba kwa wakulima kutoka wilaya tano mkoani hapo zilichaguliwa kulima zao ili waweze kuzalisha pamba nyingi na nzuri kwa ajili viwanda mbalimbali hapa nchini.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana wilayani Igunga wakati alipokwenda kujionea hali halisi ya Kiwanda cha Pamba cha Manonga wilayani Igunga ambacho kimekuwa hakifanyi kazi kwa miaka zaidi ya 20 kwa sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa pamba ya kutosha.

Alisema kuwa watendaji wote wanaohusika na usimamizi wa zao la pamba ni vema wakahakikisha kuwa wakulima wanapanda mbegu zinazotakiwa na kwa nafasi inayoshauri kitaalamu na kutimia mbolea na dawa za kuua wadudu zinazotakiwa.

Mwanri alisema kuwa Tabora imepata mbegu bora tani 500 ambazo zitasaidia kusambazwa katika Wilaya ambazo zimechaguliwa kulima zao la Pamba za Kaliua, Urambo, Nzega, Igunga na Uyui.

Alisisitiza pamba itakayolimwa na kuvuna itauzwa kupitia Vyama vya Ushirika na sio vinginevyo ili kuepuka mkulima kunyonywa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alipiga marufuku matumizi ya mbegu ambazo hazikuidhinishwa na Bodi ya Pamba na kuingiza mkoani hapa dawa ambazo zimepitwa na wakati.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (mwenye shati jeupe ) akiongozana na viongozi mbalimbali kukagua mitambo ya Kiwanda cha Pamba cha Manonga jana wilayani Igunga kwa ajili ya kujionea hali halisi kilivyo hivi na mahitaji yake ili kianze upya uzalishaji.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...