Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kushoto) na Mkurugenzi wa Twende App Justin Kashaigili (kulia) wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma mpya ya simu za mkononi ijulikanayo kama Twende App inayiowawezesha wasari kupata huduma ya haraka na usalama ya usafiri wa umma wa Taxi, pikipiki za bodaboda na pikipiki za magurudumu matatu kwa kutumia simu za mkononi.


Kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali nchini, Tigo Tanzania imeungana na kampni inayotoa huduma za usafiri Twende App kuzindua huduma mpya itakayowezehsa wasafiri kupata huduma bora, ya haraka na uhakika zaidi kupitia mfumo wa simu za mkononi unaojulikana kama Twende App. 



TwendeApp ni mfumo wa kidigitali wa simu za mkononi unaowezesha wasafiri kutafuta na kupata usafiri wa taxi, pikipiki za magurudumu mawili (bodaboda) na zile za magurudumu matatu kupitia simu zao za mkononi kwa uhakika zaidi na kwa bei nafuu. 



Twende App ambayo, tayari inatumika katika jiji la Dar es salaam, sasa imepanua wigo wake na kufikia miji ya Arusha, Morogoro, Mwanza, Kilimanjaro, Dodoma Iringa na Mbeya. Kuna mipango ya kusambaza huduma hiyo kwenda Zanzibar, Tanga na Mtwara. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...