Mkufunzi Nuria Mshare akitoa mada kuhusu ushawishi na utetezi kwa maafisa miradi wa asasi za vijana kuhusu namna ya kufanya shughuli ushawishi, utetezi na ufuatiliaji wa haki za vijana katika ngazi ya serikali za mitaa, kitaifa na kimataifa kwenye mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Saddam Khalfan (Afisa wa Program - UNA Tanzania) akielezea kuhusu sera ya maendeleo ya vijana ya mwaka 2007 na mchakato wa kupitia upya sera hiyo na mchakato wa kukusanya maoni ya sera ya maendeleo ya vijana kwenye mkutano uliowakutanisha asasi mbalimbali za vijana kutoka Tanzania Bara na Visiwani chini ya ufadhili wa The Foundation for Civil Society ili kuwajengea uwezo katika ushawishi na utetezi na ufuatiliaji wa haki za Vijana.
Rais Wa Chama ca Walimu wenye Uziwi(CWUT), Theresia Nkwera(kulia) akipata ufafanuzi wa mafunzo kwa vitendo kutoka kwa Bi Eliza William wakati wa uwasilishwaji wa mada kuhusu usashwishi na utetezi kwa maafisa miradi wa asasi za vijana kuhusu namna ya kichambua sera ya maendeleo ya vijana ya mwaka 2007 na mchakato wa kupitia upya sera.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...