Mkadiriaji majenzi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Qs. Judith Aron, akizungumza na wanafunzi wa kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Mahiwa iliyopo kata ya Nyango mkoani Lindi, kuhusu faida za usomaji wa masomo ya Sayansi na Hisabati.
Wanafunzi wa kidato cha Tano na Sita wa Shule ya Sekondari Mahiwa iliyopo kata ya Nyango mkoani Lindi, wakimsikiliza mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi Liberatha Alphonce (hayupo pichani), wakati akiwasilisha mada ya umuhimu wa masomo ya sayansi na hisabati kwa Taifa na Dunia kwa ujumla.
Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha Alphonce, akifafanua jambo kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Mtama iliyopo mkoani Lindi wakati akitoa mada kuhusu uhamasishaji wa masomo ya Sayansi na Hisabati kwa wasichana.
Mwanafunzi pekee wa kike wa kidato cha nne anayesoma masomo ya Sayansi, Saumu Abdallah, akitoa maoni yake kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara kuhusu changamoto zinazokabili shule yao.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mtama mkoani Lindi, Bi. Asha Namjupa, akisisitiza jambo kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara kuhusu mipango walionao katika kuhamasisha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya Sayansi na Hisabati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...