Ilikuwa ni siku ya furaha mno kwa wananchi wa jamii ya wafugaji kitongoji cha Endevesi, kata ya Njoro, Wilayani Same. Ambapo Septemba 12, 2017 wakati Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Rosemary Senyamule akipokea majengo ya Shule ya msingi kwa niaba ya serikali. Pamoja Na mradi wa Maji kwa ajili ya wananchi hao wasiopungua 6,000. Shule hiyo yenye madarasa 6, ofisi za walimu, vyoo Na nyumbani za walimu. Imejengwa kwa ushirikiano wa masista wa Grail, Joy of faith Na Korea Hope Foundation. 
 
Jamii hii ya Endevesi walikuwa wakipata Huduma hizi umbali wa km. Zaidi ya 5 Na kupelekea watoto wengi kuwa watoro. "Shule tumejengewa, serikali tutahakikisha tunapanga walimu Na shule hii inaanza 2018. Wananchi wakikishe wanaleta watoto shuleni. Nasi tutawachukulia hatua wote watakaokuwa watoro." Aliwashukuru pia kwa kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wa Tanzania katika kuhimiza elimu. Miradi hiyo imegharimu zaidi ya Tshs. 800M.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Rosemary Senyamule akiongea mara baada ya kupokea majengo yaliyojengwa kwa ushirikiano wa masista wa Grail, Joy of faith na Korea Hope Foundation.
Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Rosemary Senyamule akipanda mti wa 
 kumbukumbu.

  
 Mkuu wa wilaya na kiongozi wa Korea Hope Foundation wakinawa mikono katima bomba ambalo ni moja ya mradi waliokabidhiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...