Diwani wa Kata ya Matuli Halmashauri ya Morogoro Vijijini, Tafarani Ngerengere akizungumza na wananchi katika shule ya Sekondari iliyopo kwenye Kata ya Matuli. Shule hiyo ya sekondari licha ya kuwa na madarasa mawili, ofisi ya walimu na matundu manne ya vyoo yaliyokamilika lakini bado haijapata usajili na kuanza kupokea wanafunzi, hali ambayo inalalamikiwa na Diwani huyo na wananchi wa kata hiyo.
Mwananchi wa Kijiji cha Matuli kata ya Matuli akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kata ulioitishwa kujadili hatma ya sekondari yao ya kata ya Matuli.
Wananchi wa Kata ya Matuli wakimsikiliza Diwani wa Kata hiyo, Lukas Lemomo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Matuli kata ya Matuli Halmashauri ya Morogoro Viijini.
Majengo ya Shule ya sekondari ya kata ya matuli yaliyokamilika ambayo wananchi wanadai bado shule hiyo haIjapata kibali cha kufunguliwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...