Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ngugai  akisisitiza jambo wakati wa Kikao cha Bunge leo mjini Dodoma.
 aziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi akilieleza Bunge leo mjini Dodoma kuhusu mkakati wa Serikali kukamilisha ujenzi wa nyumba elfu kumi za makazi kwa askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania  (JWTZ )  ambapo kati ya hizo zaidi ya elfu sita zimeshakamilika.
 Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid (wakwanza  kulia)  akifuatilia kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo mjini Dodoma wakati wa ziara yake .
 Mbunge wa Mtwara Vijijini Mhe . Hawa Ghasia akichangia hoja Bungeni leo mjini Dodoma kuhusu maboresho katika sekta ya Afya hasa suala la tohara kwa wanaume ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupunguza  maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akisisitiza jambo mara baada ya kuwasilisha muswaada wa sheria ya marekebisho ya Sheria mbalimbali  namba 3 wa mwaka 2017 leo Bungeni mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayoshughulikia  Katiba na Sheria Mhe.  Mohamed Mchengerwa (Mb) akiwasilisha maoni ya Kamati hiyo kuhusu  muswaada wa sheria ya marekebisho ya Sheria mbalimbali  namba 3 wa mwaka 2017 leo Bungeni mjini Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu, Kazi,  Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo kwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi.
( Picha zote na Frank Mvungi- Maelezo Dodoma ).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...