Juhudi za kuopoa miili ya watu waliokuwemo kwenye gari hiyo ikiendelea.
Baadhi ya Wananchi mbalimbali wakilishuhudia tukio hilo la kuzama kwa gari ndogo ya abiria (HIACE),ambalo namba zake za usajili hazikuweza kutambulika mara moja,mara baada ya kuopolewa ziwani.
Wananchi kutoka maeneo mbali mbali wakilifuatilia tukio hilo mapema leo Kigongo Feri jijini Mwanza
Globu ya Jamii imepokea picha na maelezo kadhaa kutoka kwa mdau aliyeko jijini Mwanza zikionesha na kueleza kutokea kwa ajali jijini humo mapema leo,amesema kuwa ajali hiyo ni ya gari ndogo ya abiria Hiace ikiwa na ibiria imepitiliza na kutumbukia ziwa Victoria katika kivuko cha kigongo feri -Busisi,Wilayani Misungwi na kusababisha vifo vya watu 12 na majeruhi wawili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...