Nchini Tanzania Matumizi ya TEHAMA yame endelea kukua katika maeneo mbali mbali. Hii ime endelea kurahisisha upatikananaji wa huduma muhimu na kuwezesha watu kuendelea kuwasiliana kwa urahisi.

Viwanda na Taasisi mbali mbali zimeendelea kutumia TEHAMA ili kukuza ufanisi na kufikia watu wengi kwa kipindi kifupi. Miamala ya kifedha, ukusanyaji kodi, pamoja na mawasiliano ni baadhi tu ya mambo yanayo wezeshwa na TEHAMA nchini.

Usalama wa mifumo ya TEHAMA ni moja ya jambo muhimu sana ambapo Tanzania inapaswa kuwekeza ili kujilinda na aina zozote za kialifu mtandao ambazo zinaweza kupelekea huduma muhimu kutopatikana na hatimae uchumi wa Nchi kuyumba.
-------------------
STATISTICS: Tanzania installed 27,000 KMS of optic fiber connecting all regions and it has 7 mobile operators – About 94% network coverage, 85% SIM penetration and 40%internet users.
-------------------
Mkutano mkuu wa mwaka wa wataalam wa TEHAMA nchini Tanzania ulio fanyika mwishoni mwa wiki iliyopita (26 – 27, Octoba – 2017) jijini Dar-es salaam ulipata kujadili usalama mtandao ambapo mada kadhaa zilizo jikita katika kutoa elimu ya namna bora za kuimarisha usalama wa mifumo yetu zili wasilishwa na kujadiliwa.

Binafsi, Nilizungumza na washiriki kuhusiana na namna bora ya kulinda taarifa zinazo patikana kwenye simu zetu na komputa mpakato (Protecting Mobile devises Data) ambapo vifaa hivi vimekua vikitumika katika utendaji wa shughuli za kiofisi na kufanya miamala ambapo taarifa hizo zimekua muhimu kulindwa dhidi yawahalifu mtandao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...