.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack.Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee mkoa wa Shinyanga, Faustine Masale Sengerema,kushoto ni Katibu mkuu wa Baraza la Ushauri la Wazee mkoa wa Shinyanga,Underson Lyimo. 
Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee mkoa wa Shinyanga, Faustine Masale Sengerema akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazee ambapo alisema wazee wanaunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli katika kuwaletea maendeleo wananchi.
Wazee wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea....
Katibu mkuu wa Baraza la Ushauri la Wazee mkoa wa Shinyanga,Underson Lyimo akisoma risala ambapo alizipongeza halmashauri zilizofanikisha zoezi la kutoa kadi za matibabu bila malipo kwa wazee zikiongozwa na halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.Aliyeshikilia kipaza sauti ni Afisa Maendeleo ya Jamii Sekretarieti ya mkoa wa Shinyanga Glory Mbia.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikabidhi kadi ya matibabu bila malipo kwa mzee Philipo Njabuga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...