Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (katikati) akizungumza na Madiwani na baadhi ya wakulima Bonde la Mwamanyili wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega (hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika Nyashimo kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili Wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mhe.Vumi Magoti(wa pili kulia)akizungumza na Madiwani na baadhi ya wakulima wa Busega(hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Nyashimo kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili Wilayani humo
Madiwani na baadhi ya Wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakifuatilia mjadala kuhusu suala la maombi ya Mkopo kwa ajili ya Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Wilayani Meatu katika kikao cha dharura cha Baraza kilichofanyika Mjini Mwanhuzi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya ya Busega (meza kuu) na baadhi ya wakulima baada ya kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani humo.

Na Stella Kalinga, Simiyu
Mabaraza ya Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega na Meatu Mkoani Simiyu yameridhia Halmashauri hizo kukopa shilingi bilioni 17.1 kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), kwa ajili ya kutekeleza Miradi mikubwa miwili ya Maendeleo.

Maridhiano hayo yamefikiwa katika Vikao vya dharura vya mabaraza ya madiwani vilivyofanyika kwa nyakati tofauti, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Busega imepanga kukopa shilingi bilioni 10.7 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili (eneo la ekari 2050)  na Meatu shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha maziwa(MEATU MILK).

 Akiwasilisha taarifa ya Maendeleo ya Mpango wa Kilimo cha Umwagiliaji Wilayani Busega, Afisa Mipango wa Wilaya hiyo Josephat Joseph, amesema hadi sasa kazi za upimaji wa mashamba na njia ya kupita bomba la maji, kupima udongo, kusanifu mfereji mkuu kwenye chanzo, sehemu ya kuchukulia maji, nyumba za pampu, mifereji ya kuingiza na kutolea maji,kuandaa michoro na gharama za mradi zimeshakamilika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...