MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amezitaka benki zote zilizopo hapa nchini kuhakikisha zinaanzisha matawi yake katika mikoa mbalimbali ili kuwawezesha wananchi hasa wanawake kupata huduma za kifedha kirahisi.
Samia ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa kimataifa wa Wanawake na Fedha uliyoandaliwa na Shirika la Kimataifa la Women’s World Banking na Benki ya NMB kuwa mshirika mwenza katika mkutano huo.
Mkutano huo ambao kwa mara ya kwanza umefanyika barani Afrika, nchini Tanzania umewakutanisha pamoja wanawake viongozi katika fani mbalimbali zaidi ya 300, zikiwemo mabenki, teknolojia, wafanyabiashara, mashirika ya umma na binafsi.
Mama Samia alisema benki zinapaswa kwenda zaidi kwa wananchi kwa kuanzisha matawi yao huko mikoani kwani baadhi ya watanzania wapo nje kabisa na mifimo ya kibenki kutokana na kutofikiwa.
“Asilimia 70 ya watanzania wanatumia simu za mkononi na kama mnavyojua Tigopesa, Mpesa na zinginezo zimesambaa sana hapa nchini hii inayonyesha huduma za kifedha tumepiga hatua ingawa bado kuna mambo tunapaswa kurekebisha kwa mfano mabenki yetu yaendelee zaidi kwenda huko kwa wananchi kwa kufungua matawi mengi.
Lakini pia benki yetu ya Wanawake ambayo imeundwa kwa madhumuni hayo tunaitaka ijitahidi kusambaza matawi yake huko mikoani, hivyo mkutano huu utaangalia ni jinsi gani jamii inafikiwa zaidi na huduma za kifedha hasa wanawake walioko vijijini ili wapate huduma za fedha ambazo ndizo zinakuza uchumi wan chi,” alisema.
Aidha alisema Shirika la Kimataifa la Women’s World Banking wameamua kuja kufanya kongamano hilo kwa mara ya kwanza hapa nchini ili kuja kuangalia Tanzania inafanyaje katika kusaidia maendeleo ya wanawake.
Naye Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wa Kati wa Benki ya NMB, Abdumajid Nsekela alisema mkutano huo uliowakutanisha watu mbalimbali utajikita zaidi kuangalia ni kwa jinsi gani wataweza kumuwezesha mwanamke kupata fursa ili aweze kujikwamua kwenye mitaji na uwekezaji.
Alisema Benki ya NMB imeshirikiana kwa karibu na shirika hilo la Women’s World Banking katika kuzalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo ya kuwawezesha wananchi kwa maana ya mkulima na wafanyakazi hasa wanawake kwa kutengeneza bidhaa ambazo zitawawezesha kupata mikopo nafuu pamoja na kufungua akaunti.
“Zaidi ya wadau 300 ambao wametoka katika nchi mbalimbali duniani wapo katika mkutano huu wanajadiliana ni jinsi gani watumie teknolojia kumfikia mtanzania kwa ukaribu zaidi, wanawake wengi waliopo vijijini ni wakulima na wanahitaji huduma za kifedha hivyo mkutano huu ni mahususi kujadiliana changamoto zinazokwamisha kuwafikia wanawake


Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akifungua mkutano wa taasisi ya benki ya ulimwengu ya kusaidia maendeleo ya wanawake uliofanyika jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Benki ya NMB. (Picha na Francis Dande).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemeker, akiongea baada ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kufungua mkutano wa Kimataifa la Women’s World Banking uliofanyika jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Benki ya NMB.


Washiriki a mkutano wa kimataifa wa Women’s World Banking.


  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...