Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii
Kampuni ya Msama Auction Mart imempongeza Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kwa kauli yake kuhusu wizi wa kazi za sanaa nchini.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Alex Msama amesema kuwa Kampuni yao imeona kuwa Waziri huyo ameonesha nia yakupoteza kabisa kazi feki za Sanaa.
Hatua hiyo ya Waziri pia itawagusa wenye kazi zao ambao ni Wasanii wa kazi hizo ikiwemo Wasanii wa Bongo Fleva, Nyimbo za Injili, Maigizo na Filamu.
Msama amesema kuwa doria za kumaliza wizi huo wa kazi za Wasanii inaendelea kwa nchi nzima, ambapo Mkoa mmoja tu ndiyo wenye ahueni yakupunguza wizi huo ambao ni Mwanza.
"Msama Auction Mart kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo inategemea kuanza zoezi lakumaliza kazi feki za sanaa nchini, zoezi ambalo lisilokuwa na mwisho", amesema Msama.
Pia Msama ameonya wale wote wanaofanya biashara za kuuza kazi feki, ambapo amesema kuwa watakapokamata Kompyuta za kufanyia kazi hizo basi hazitarudi tena kwa wahusika.
Wafanyabiashara wa Filamu za Nje nao wametakiwa kuacha kufanya biashara hizo bila kibali cha mwenye kazi husika, kwani hatua hiyo inaikosesha Serikali mapato.
Kampuni ya Msama Auction Mart imempongeza Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kwa kauli yake kuhusu wizi wa kazi za sanaa nchini.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Alex Msama amesema kuwa Kampuni yao imeona kuwa Waziri huyo ameonesha nia yakupoteza kabisa kazi feki za Sanaa.
Hatua hiyo ya Waziri pia itawagusa wenye kazi zao ambao ni Wasanii wa kazi hizo ikiwemo Wasanii wa Bongo Fleva, Nyimbo za Injili, Maigizo na Filamu.
Msama amesema kuwa doria za kumaliza wizi huo wa kazi za Wasanii inaendelea kwa nchi nzima, ambapo Mkoa mmoja tu ndiyo wenye ahueni yakupunguza wizi huo ambao ni Mwanza.
"Msama Auction Mart kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo inategemea kuanza zoezi lakumaliza kazi feki za sanaa nchini, zoezi ambalo lisilokuwa na mwisho", amesema Msama.
Pia Msama ameonya wale wote wanaofanya biashara za kuuza kazi feki, ambapo amesema kuwa watakapokamata Kompyuta za kufanyia kazi hizo basi hazitarudi tena kwa wahusika.
Wafanyabiashara wa Filamu za Nje nao wametakiwa kuacha kufanya biashara hizo bila kibali cha mwenye kazi husika, kwani hatua hiyo inaikosesha Serikali mapato.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...