NA YEREMIAS NGERANGERA -NAMTUMBO

Wanachama wa chama cha mapinduzi wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma wamemchagua Aggrey Mwansasu kuwa mwenyekiti mpya wa chama hicho kwa kumbwaga aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Benjamini Nindi .

Uchaguzi wa kumpata mwenyekiti huyo ulifanyika katika Bwalo la shule ya sekondari Namtumbo shule ambayo inamilikiwa na jumuiya ya wazazi wa chama cha mapinduzi kilomita tatu kutoka mjini Namtumbo.

Aidha katika uchaguzi huo awali uliingia dosari baada ya msimamamizi wa uchaguzi huo Zena Rashidi Mijinga kujisahau kwa kutosoma kanuni ya kushinda uchaguzi ni sharti mgombea apate asiliomia hamsini ya kura zitakazopigwa.

Dosari ya kanuni hiyo kutosomwa awali ilijionesha baada ya wagombea wa nafasi ya uenyekiti kutofikia asilimia hamsini ya kura zilizopigwa na kuwataka wajumbe wa mkutano huo kurudia kupiga kura kwa nafasi ya uenyekiti hali iliyoibua hasira kutoka kwa wajumbe kwa madai ya kutaka kumbeba mgombea mmojawapo katika uchaguzi huo na kuongeza kuwa kanuni hizo kwa nini hazikusomwa kabla ya uchaguzi na badala yake zisomwe wakati uchaguzi umefanyika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...