Na Fredy Mgunda,Iringa.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa
wa Kihesa Kilolo B kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Eden
Madembo amempigia magoti mbunge wa viti maalumu mkoa wa Iringa Ritta Kabati
kuwasaidia kukarabati shule ya msingi Igeleke kwa kuwa miundo mbinu yake
imeharibika na sio rafiki kwa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo.
Akizungumza na blog bwana
Madembo alisema shule hiyo inamiundombinu mibovu hivyo ni hatarishi kwa wanafunzi
wa shule hii kwanza toka mwaka 1978 hadi leo shule hiyo haijawahi kufanyiwa
ukarabati wa kueleweka hivyo inahitajika kukarabatiwa haraka iwezekanavyo.
“Mwandishi ukiangalia
majengo ya shule hii unaona jinsi gani yalivyoaribika na ipo katika halmashauri
ya manispaa ya Iringa lakini viongozi wengi hawaingalii kwa jicho la tatu kitu
kinachotupa shida sisi viongozi wa eneo hili” alisema Madembo
Madembo alisema kuwa shule
nyingi zilizojengwa miaka ya 1978 na kuendelea zinamiundombinu ilichoka hivyo
serikali na viongozi wa kisiasa kuanza kuzitafutia mikakati ya kuzikarabati ili
kuboresha taaluma kwa watoto wetu kuendana na karne ya sasa.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kihesa Kilolo B kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Eden Madembo akiwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati wakati wa kuzitambua changamoto zinazoikabili shule ya msingi Igeleke iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Iringa
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kihesa Kilolo B kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Eden Madembo akiwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati wakiwa katika picha nawanafunzi wa darasa la saba
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa na viongozi mbalimbali wakikagua madarasa ambayo miundombinu yake imeharibika.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...