Abrahamu Too kutoka Kenya ameibuka mshindi wa
kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza jana
baada ya kumaliza kwa muda wa saa 02:22:45, akifuatiwa kwa karibu na mshiriki
mwenzake kutoka nchini humo Moris Motima aliyetumia muda wa saa 02:23:19
Kivutio katika mbio hizo
ilikuwa ni Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza ambae
mbali na kuzindua mbio hizo pia alishiriki katika mbio za km 3 akiambatana na
viongozi wengine wa serikali.
Nafasi ya tatu katika mbio
hizo pia ilichukuliwa Mkenya George Onyacha aliyetumia muda wa saa 02:23:27,
ikiwa sekunde chache nyuma ya mpinzani wake.
Katika mbio hizo zilizoanzia
na kuhitimishwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini humo ilishuhudiwa nafasi ya kwanza
hadi ya saba zikishikwa na wakimbiaji kutoka nchini Kenya huku nafasi ya nane
ikienda kwa Mtanzania Paschal Mombo alietumia muda wa saa 02:30:43.
Akizungumzia siri ya ushindi
wake, mbali na kusifia uratibu mzuri wa mbio hizo uliomuwezesha kukimbia bila
changamoto yoyote Too alisema ni kujituma kufanya zaidi mazoezi na kukaa
kambini muda mrefu ili kufanya vizuri katika michuano ya mwaka huu.
“Maandalizi ya mwaka huu ni
mazuri na washiriki wameendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka jambo linalotufanya
wanariadha kujiwekea mikakati mizuri ili kuweza kukabiliana na ushindani mkali
uliopo katika mbio hizi na ninashukuru Mungu nimefanikiwa,” alisema.
Abrahamu Too kutoka Kenya
akimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika
jijini Mwanza jana baada ya kumaliza kwa muda wa saa 02:22:45, akifuatiwa kwa
karibu na mshiriki mwenzake kutoka nchini humo Moris Motima aliyetumia muda wa
saa 02:23:19.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa
na Michezo, Bi Juliana Shonza akizungumza na waandishi wa habari kabla ya
kuzindua mbio za Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza jana ambapo alikimbia mbio za km 3 akiambatana na
viongozi wengine wa serikali.
Mbali na washiriki kutoka
ndani ya nchin pia pia washiriki kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo China na
Marekani nao hawakuwa nyuma.
Rais wa Shirikisho la riadha
nchini (RT) ambae pia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bw Anthony Mtaka akizungumza
kwenye warsha ya kukabidhi zawadi kwa washindi ambapo pamoja na mambo mengine
aliwapongeza waandaaji wa mbio hizo kampuni ya Capital Plus Internantional
(CPI).
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa
na Michezo, Bi Juliana Shonza ( katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na
washindi wa kwanza hadi wa tatu wa mbio za Km 42 (waliosimama nyuma) mara baada
ya kuwakabidhi zawadi pamoja na medali. Wengine ni pamoja na Rais wa Shirikisho
la riadha nchini (RT) ambae pia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bw Anthony Mtaka(wa
tatu kushoto), waandaaji pamoja na viongozi wa mchezo huo.
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa
na Michezo, Bi Juliana Shonza (Kushoto) akikabidhi zawadi kwa washindi wa mbio
za Km 42 kwa upande wa wanawake ambapo washindi wa kwanza hadi watano wote
walitoka nchini Kenya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...