Serikali
imetenga shilingi milioni 700 milioni kwa ajili ya kuanzisha mradi wa
maji kwenye Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara
utakaopunguza kero ya maji kwenye eneo hilo.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Isack Kamwelwe ameyasema hayo kwenye ziara yake ya siku moja Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Waziri Kamwelwe alisema radi huo wa maji utasababisha asilimia 85 ya wananchi wa mji huo kupata maji ya uhakika.
Alisema mradi huo unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani fedha za mradi huo zimeshatengwa tayari. limuagiza meneja wa mamlaka ya maji safi Babati (Bawasa) mhandisi Idd Msuya kuhakikisha mradi huo wa Mirerani unaanza na kukamilika ndani ya muda wa miezi sita.
"Baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara yake hivi karibuni kwenye mji mdogo wa Mirerani alitoa ahadi ya kupatiwa maji wananchi wa eneo hilo hivyo nikiwa Waziri mwenye dhamana hiyo amehakikisha agizo hilo limetekelezwa," alisema Waziri Kamwelwe. Alisema baada ya Rais Magufuli kuagiza maji ya uhakika yapatikane Mirerani na zoezi la ujenzi wa ukuta wa kuzunguka machimbo ya Tanzanite kuanza, yeye kama Waziri aliamua ashughulikie suala la maji Mirerani.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Isack Kamwelwe ameyasema hayo kwenye ziara yake ya siku moja Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Waziri Kamwelwe alisema radi huo wa maji utasababisha asilimia 85 ya wananchi wa mji huo kupata maji ya uhakika.
Alisema mradi huo unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani fedha za mradi huo zimeshatengwa tayari. limuagiza meneja wa mamlaka ya maji safi Babati (Bawasa) mhandisi Idd Msuya kuhakikisha mradi huo wa Mirerani unaanza na kukamilika ndani ya muda wa miezi sita.
"Baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara yake hivi karibuni kwenye mji mdogo wa Mirerani alitoa ahadi ya kupatiwa maji wananchi wa eneo hilo hivyo nikiwa Waziri mwenye dhamana hiyo amehakikisha agizo hilo limetekelezwa," alisema Waziri Kamwelwe. Alisema baada ya Rais Magufuli kuagiza maji ya uhakika yapatikane Mirerani na zoezi la ujenzi wa ukuta wa kuzunguka machimbo ya Tanzanite kuanza, yeye kama Waziri aliamua ashughulikie suala la maji Mirerani.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza juu ya
utekelezaji wa miradi mitatu ya maji kwenye Wilaya ya Simanjiro Mkoani
Manyara, (kushoto) ni Mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na
kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Jackson Leskar
Sipitieck.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...