Serikali imetenga shilingi milioni 700 milioni kwa ajili ya kuanzisha mradi wa maji kwenye Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara utakaopunguza kero ya maji kwenye eneo hilo.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Isack Kamwelwe ameyasema hayo kwenye ziara yake ya siku moja Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Waziri Kamwelwe alisema radi huo wa maji utasababisha asilimia 85 ya wananchi wa mji huo kupata maji ya uhakika.

Alisema mradi huo unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani fedha za mradi huo zimeshatengwa tayari. limuagiza meneja wa mamlaka ya maji safi Babati (Bawasa) mhandisi Idd Msuya kuhakikisha mradi huo wa Mirerani unaanza na kukamilika ndani ya muda wa miezi sita.

"Baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara yake hivi karibuni kwenye mji mdogo wa Mirerani alitoa ahadi ya kupatiwa maji wananchi wa eneo hilo hivyo nikiwa Waziri mwenye dhamana hiyo amehakikisha agizo hilo limetekelezwa," alisema Waziri Kamwelwe. Alisema baada ya Rais Magufuli kuagiza maji ya uhakika yapatikane Mirerani na zoezi la ujenzi wa ukuta wa kuzunguka machimbo ya Tanzanite kuanza, yeye kama Waziri aliamua ashughulikie suala la maji Mirerani. 
Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza juu ya utekelezaji wa miradi mitatu ya maji kwenye Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, (kushoto) ni Mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Jackson Leskar Sipitieck. 

 Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Zuwena Omary akisoma taarifa ya Wilaya hiyo kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe.
 Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mhandisi Zephania Chaula akimshukuru Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe kwa utekelezaji wake wa miradi ya maji Simanjiro. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...