Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya Peoples Media inayoendesha Kituo cha Radio cha Uhuru FM cha Jijini Dar es Salaam, Paul Mng'ong'o (wanne kushoto), akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula kwa Mwanzilishi wa Kituo cha kujeresha katika maisha ya kawaida waraibu wa dawa za kulevya cha Pili Misana Foundation, Pili Misana, kilichopo Kigamboni, dar es Salaam, leo, ikiwa ni mwendelezo wa Uhuru FM kutoa misaada kupitia kampeni yao ya 'Gusa Maisha yao' kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere. Wengine katika picha ni baadhi ya wafanyakazi wa Uhuru FM na Vijana wanaoishi katika kituo hicho.
Aina ya msaada uliotolewa
Dereva akiliungurumisha basi kupitia daraja la Kigamboni kwenda kwenye kituo hicho

Baadhi ya wafanyakazi wa Uhuru FM wakiwa katika basi kwenda kwenye kituo hicho cha kusaidia waraibu wa dawa za kulevya kurejea katika maisha ya kawaida, baada ya kufika wafanyakazi hao wakaanza kushuka na vitu vya msaada, mmoja baada ya mwingine .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...