Wananchi wa Halmashauri ya mji Geita, mkoani Geita wameendelea kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la usajili na utambuzi linaloendeshwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa. Zoezi hili ambalo kwa sasa linaendelea mikoa yote ya Kanda ya Ziwa na Kaskazini limekuwa ni fursa nzuri na muhimu kwa wananchi kusajiliwa na kuwezeshwa kushiriki katika shughuli za maendeleo kutokana na umuhimu wa taarifa zinazokusanywa.

Pindi mfumo huu utakapokamilika wananchi watawezeshwa kupata huduma mbalimbali kwa urahisi pamoja na kusaidia Serikali kuimarisha Ulinzi na Usalama wa nchi kwani Kitambulisho hiki kitakuwa ufunguo kwa mifumo mingine ya Serikali kubadilishana taarifa.
Wananchi wa mtaa wa Station kata ya Mtakuja Halmashauri ya Mji Geita katika foleni wakisubiri kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa, wakati wa zoezi la usajili linaloendelea mkoani humo.
Wananchi kata ya Bulela Halmashauri ya Mji Geita wakisubiri huduma ya usajili wakati wa zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa linaloendelea Mkoani Geita.
Wananchi kata ya Bulela Halmashauri ya Mji Geita wakisubiri huduma ya usajili wakati wa zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa linaloendelea Mkoani Geita.
Afisa Msajili Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, akiendelea na zoezi la usajili Vitambulisho vya Taifa kwa Wananchi wa mtaa wa Station kata ya Mtakuja Halmashauri ya Mji Geita.
Maafisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wakiendelea na zoezi la uingizaji wa taarifa za wananchi katika zoezi la usajili Vitambulisho vya Taifa linaloendelea katika Halmashauri ya Mji Geita Mkoani Geita.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uratibu Ofisi za wilaya Bi. Rehema Kionaumela akitoa maelekeza kwa Maafisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Mkoani Geita kuhusu taratibu mbalimbali wakati wa maandalizi ya zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa Halmashauri ya Mji Geita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...