Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Baada ya kukaa gerezani kwa siku tano, leo vigogo wawili wa zamani wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) wameachiwa huru baada ya kukamilisha masharti ya dhamana waliyopewa ma Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Washtakiwa hao ambao wametimiza masharti ya na kuachiwa kwa Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba ni, Kaimu Mtendaji wa (TIA), Shaha Hanzuruni na Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Onesphor Luhungu wa Hakimu Mkazi Mkuu,


Katika masharti yao ya dhamana kila mshtakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atasaini bondi ya milioni 250 na pia mdhamini mmoja kati ya wadhamini hao kuwasilisha fedha taslimu mahakamani Sh 250 milioni ama hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha na kwamba mali hiyo ni lazima iwepo Dar es Salaam.

Mbali na hayo kila mshtakiwa alitakiwa kusalimisha pasi yake ya kusafiria mahakamani na wasitoke nje ya jiji la Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha Mahakama.

Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 24,2017 ambapo washtakiwa hao watasomewa maelezo ya awali (PH).Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha hasara ya Sh 1, 097,681,107.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...