Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Mbagala,  Sady Mwang’onda (wa pili kulia) na Meneja Bidhaa za Uwekezaji wa benki hiyo, Dorothea Mabonye (wanne kushoto), wakikata utepe kuashirikia uzinduzi rasmi wa kampeni ya akaunti ya malengo ya NBC. Kampeni hiyo itakayodumu kwa muda wa miezi mitatu na kufanyika nchini kote itashuhudia washindi sita wakijishindia kila mmoja gari jipya aina ya Suzuki Carry ‘kirikuu’ lenye thamani ya shs milioni 30. Washindi wengine 24 watajishindia kila mmoja zawadi ya pesa taslimu shs milioni moja hivyo kufanya jumla ya zawadi zote kufikia thamani ya shs milioni 204. Hafla hiyo ilifanyika katika tawi hiyo, Dar es Salaam leo. Wengine ni baadhi ya maofisa wa benki hiyo.
 Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Mbagala,  Sady Mwang’onda (katikati), Meneja wa Bidhaa za Uwekezaji wa benki hiyo, Dorothea Mabonye (kulia kwake), na Mkuu wa  Bidhaa na Wateja Rejareja, Andrew Lyimo (kushoto kwake), pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo wakishangilia mara baada ya uzinduzi rasmi wa kampeni ya akaunti ya malengo ya NBC uliofanyika katika tawi hilo, Dar es Salaam leo. Kampeni hiyo itakayodumu kwa muda wa miezi mitatu na kufanyika nchini kote itashuhudia washindi sita wakijishindia kila mmoja gari jipya aina ya Suzuki Carry ‘kirikuu’ lenye thamani ya shs milioni 30. Washindi wengine 24 watajishindia kila mmoja zawadi ya pesa taslimu shs milioni moja.
  Mkuu Bidhaa na Wateja Rejareja wa Benki ya NBC, Andrew Lyimo (katikati), akihojiwa na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari mara baada ya uzinduzi rasmi wa kampeni ya akaunti ya malengo ya NBC uliofanyika katika tawi Mbagala nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam leo. Kampeni hiyo itakayodumu kwa muda wa miezi mitatu na kufanyika nchini kote itashuhudia washindi sita wakijishindia kila mmoja gari jipya aina ya Suzuki Carry ‘kirikuu’ lenye thamani ya shs milioni 30. Washindi wengine 24 watajishindia kila mmoja zawadi ya pesa taslimu shs milioni moja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...