Afisa Magereza Bwana Neuro Mbwilo amejishindia dau kubwa kuwahi kutolewa na Tatu Mzuka la shilingi milioni 110 kupitia Mzuka jackpot iliyoonyeshwa kupitia vituo mbalimbali vya runinga nchi nzima siku ya Jumapili ya Tarehe 29 Nov 2017.

Kama ma milioni ya wachezaji wengine nchini Tanzania, Mbwilo alidhani ilikuwa ni fursa nzuri kutumia Shilingi 500 kubadilisha maisha yake pamoja na familia milele.

Bwana Mbwilo, ambaye ni Askari gereza wilayani Temeke alielezea mshtuko wake juu ya bahati iyo iliyomtembelea. "Ni hisia ambayo haielezeki kabisa. Nina furaha kubwa sana, nimejawa na shukrani nyingi,na kwangu hii ni ajabu kabisa ", alielezea mbele ya vyombo vya habari.

Katika kutoa hundi ya ushindi huo wa milioni 110 Bwana Sebastian Maganga, Meneja wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka alielezea zaidi juu ya ushindi huo mkubwa lakini aliwakumbusha Watanzania kwamba kuna njia nyingi za kushinda kupitia Tatu Mzuka. Alifafanua kuwa katika wiki 13 tu Tatu Mzuka imetengeneza zaidi ya washindi milioni 2 na kutoa billion 4 kwa washindi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva ( Kushoto)  akimkabidhi Mfano wa hundi ya sh Milioni 110 Ofisa ya Jeshi la Magereza Neuro Mbwilo, ambaye ni mshindi wa bahati nasibu ya Mzuka jackpot, Dar es Salaam.
 Mshindi wa millioni 110 Bwn. Mbwilo akiwa na washkaji zake wawili Juma Athuman na Joseph Haule Walio zawadia  milioni moja moja na Tatu Mzuka kwenye promotion ya "Cheza na Washkaji na Shinda na Washkaji".
  Bwana Mbwilo akisherekea ushindi wake na Mke wake Nyumbani kwao Keko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...