Shamba darasa hilo litatumika kama darasa la kilimo cha pamba kwa njia za kitaalamu kwa wakulima wa pamba katika wilaya hiyo katika msimu hu wa kilimo cha pamba ili waweze kuvuna mazao mengi na kujiongezea kipato pia kuondokana na uhaba wa chakula.   
DC Matiro ambaye alikuwa ameambatana na wataalamu pamoja na viongozi wa kata ya Solwa ,mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bakari Mohamed Novemba 24,2017,amepanda zao la pamba kwenye shamba darasa la kata hiyo.  
Akizungumza wakati wa kupanda pamba katika shamba hilo Matiro aliwataka wakulima wa halmashauri hiyo kuiga mfano wa kilimo cha kitaalamu kinachofanywa kwenye mashamba darasa kwa kutumia kamba. “Lengo la mimi kuingia shambani na kuanza kupanda zao la pamba pamoja na viongozi wa kata hii ni kuhamasisha wakulima kulima kitaalamu ili waweze kupata mavuno mengi kwani wakizembea hakuna wa kuwaletea chakula na serikali haina shamba hivyo wajitahidi kufuata maelekezo ya wataalamu ili kujiinua kiuchumi kupitia zao hili la biashara”,alisema Matiro.  
Hata hivyo alisema katika msimu huu wa kilimo cha pamba serikali imejitahidi kuleta mbegu bora za aina zote kwa wakulima. Matiro alisisitiza kila kata iwe na shamba darasa litumike kama mfano kwa wakulima na kila shule kupanda zao la mtama kwa wingi. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameshiriki katika kilimo cha pamba katika shamba darasa lililoanzishwa katika kijiji cha Solwa kata ya Solwa katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...