Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo amesema hatavumulia kuwa na watumishi mizigo ambao hawatimizi majukumu yao kikamilifu na kuleta mabadiliko katika sekta ya barabara ambayo ni nguzo ya uchumi nchini.
Waziri Jaffo ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wabunge wa Kamati ya kudumu Serikali za mitaa(TAMISEMI) sambamba na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa(LAAC) kuhusu majukumu ya Wakala wa barabaraza vijijini na mijini(TARURA) iliyofanyika katika ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma
Mhe. Jaffo amesema Serikali ilishatoa muongozo wa malengo ya utendaji kazi katika utumishi wa umma na kuwapima kulingana na malengo yao hivyo watumishi ambao watashindwa kutekeleza na kufikia malengo waliyopangiwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kiutumishi.
Amesema kuwa Serikali haitavumilia suala zima la ubadhilifu kwa watumishi wa umma, kwa kuwa Serikali haiwezi kumbeba mtu ambaye ni mbadhilifu kwa kuwa Serikali inahitaji kuleta mabadiliko katika utendaji kazi na kuleta maendeleo kwa jamii.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo akiongea kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya bunge ya utawala na Serikali za mitaa na kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini Mhandisi Victor Seif akieleza majukumu ya TARURA kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya bunge ya utawala na Serikali za mitaa na kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini Bw.Abdul Digaga akiongea kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya bunge ya utawala na Serikali za mitaa na kamati ya kudumu ya bunge ya hesabu za Serikali za Mitaa kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina mjini Dodoma.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...