NA DENIS MLOWE, IRINGA
MBUNGE
Wa viti maalum Mkoa Wa Iringa, Ritta Kabati ametoa wito kwa jamii
kuondoka na itikadi za kisiasa pindi linapokuja suala la maendeleo kwa
wananchi.
Akizungumza
na wazazi na walezi wa shule ya msingi Igeleke wakati wa ukarabati wa
madarasa ya shule hiyo mwishoni mwa wiki ikiwa ni ahadi yake ya
kukarabati shule za msingi zenye miundo mbinu mibovu na zamani, Kabati
alisema kuwa suala la ujenzi wa madarasa hauna siasa.
Alisema
kuwa maamuzi ya kukarabati shule za msingi lengo ni kuyaweka mazingira
bora ya kusomea wanafunzi na kuwaepusha na ajali zinazoweza kujitokeza
kutokana na uchakavu wa majengo.
Kabati
alisema kuwa imekuwa kawaida pindi mtu akitaka kufanya maendeleo mambo
ya siasa yanaingizwa ila kwa serikali hii ya hapa kazi lazima tufanye
kazi za kuleta maendeleo kwa wananchi.
Kabati (mwenye njano) akishirikiana na wananchi kubeba zege kwa ajili ya ukarabati wa shule ya msingi Igeleke
Kabati (mwenye njano) akishirikiana na wananchi kubeba zege kwa ajili ya ukarabati wa shule ya msingi Igeleke
Mbunge
wa viti maalum Ritta Kabati akikabidhi saruji kwa uongozi wa shule
kabla ya kuanza ukarabati katika shule ya msingi Igeleke.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...