NA DENIS MLOWE, IRINGA

MBUNGE Wa viti maalum Mkoa Wa Iringa, Ritta Kabati ametoa wito kwa jamii kuondoka na itikadi za kisiasa pindi linapokuja suala la maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza na wazazi na walezi wa shule ya msingi Igeleke wakati wa ukarabati wa madarasa ya shule hiyo mwishoni mwa wiki ikiwa ni ahadi yake ya kukarabati shule za msingi zenye miundo mbinu mibovu na zamani, Kabati alisema kuwa suala la ujenzi wa madarasa hauna siasa.

Alisema kuwa maamuzi ya kukarabati shule za msingi lengo ni kuyaweka mazingira bora ya kusomea wanafunzi na kuwaepusha na ajali zinazoweza kujitokeza kutokana na uchakavu wa majengo.

Kabati alisema kuwa imekuwa kawaida pindi mtu akitaka kufanya maendeleo mambo ya siasa yanaingizwa ila kwa serikali hii ya hapa kazi lazima tufanye kazi za kuleta maendeleo kwa wananchi.
Kabati (mwenye njano) akishirikiana na wananchi kubeba zege kwa ajili ya ukarabati wa shule ya msingi Igeleke
Kabati (mwenye njano) akishirikiana na wananchi kubeba zege kwa ajili ya ukarabati wa shule ya msingi Igeleke
 Mbunge wa viti maalum Ritta Kabati akikabidhi saruji kwa uongozi wa shule kabla ya kuanza ukarabati katika shule ya msingi Igeleke.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...