Askofu Mkuu wa Kanisa la Christ Chapel la nchini Canada, Jacob Afolabi akiongoza ibada maalum ya kiswahili ya kuombea Amani kwa Tanzania pamoja na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Uchumi na Uwekezaji Makini, iliyofanyika katika kanisa hilo, Novemba 5, 2017 Ottawa nchini Canada . Ibada hiyo pia ilihudhuliwa na Balozi wa Tanzania nchini humo, Balozi Jack Mugendi Zoka aliyeambatana na Mkewe pamoja na Watanzania wengine waishio nchini humo. Ibada hiyo iliangaliwa na Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Canada.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Good News for All, Charles Gadi alikuwa ni mmoja wa Maaskofu walioongoza Ibada hiyo, iliyofanyika katika kanisa la Christ Chapel lililopo, Ottawa nchini Canada
Balozi wa Tanzania nchini Canada, Balozi Jack Mugendi Zoka aliyeambatana na Mkewe wakishiriki Ibada hiyo.
Balozi wa Tanzania nchini Canada, Balozi Jack Mugendi Zoka akiwa katika picha ya pamoja na Waumini wa Ibada hiyo ambao ni Wanajumuiya ya Watanzania waishio nchini humo, wakiwa wameshika picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
Balozi wa Tanzania nchini Canada, Balozi Jack Mugendi Zoka akibadilishana mawazo na Bw. John Kalonga ambaye ni Mmoja wa Watanzania waishio nchini humo, baada ya kumalizika kwa ibada hiyo. Wengine pichani ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Good News for All, Charles Gadi (wa pili kulia), Mke wa Balozi (katikati) pamoja na Afisa wa Ubalozi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...