Na Karama Kenyunko blogu ya jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepokea maelezo ya onyo ya mshtakiwa Yang Feng Glan anayedaiwakuwa malikia wa tembo, ambayo yatatumika kama moja ya kielelezo katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Glan ambaye ni raia wa China na watanzania wawili.

Maelezo hayo yamepokelewa na hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi anayesikiliza kesi hio.Kabla ya kupokelewa,askari Polisi wa kikosi kazi cha taifa cha kupambana na ujangili, E.1180 Koplo Emmanuel alieleza kuwa alitumia masaa mawili kuchukua maelezo ya onyo ya mshtakiwa katika Kituo cha Polisi cha Osterbay.

Koplo Emmanuel alidai hayoleo alipokuwa akiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu,Faraja Nchimbi kutoa ushahidi katika kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi.

Amedai,Septemba 27,2015 majira ya usiku alipigiwa simu na kaimu DCI akimtaka afike Polisi Osterbay ambapo alipofika hapo alimkuta mshtakiwa Yang Feng akituhumiwa kwa kujihusisha na tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo na kutakiwa amfanyie mahojiano.

Alidai katika mahojiano mshtakiwa alijitambulisha kwa jina la Yang, akamuuliza kama anatambua kosa lake na kwamba,Yang alimueleza kuwa anatuhumiwa na kujihusisha na nyara za Serikali ambazo ni meno ya tembo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...