Naibu
Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Mheshimiwa Anthony Mavunde leo
amemkabidhi kitita cha shilingi Milioni 60 mshindi wa droo ya Tatumzuka
Bwana Robert Changadiko ambaye alijishindia kiasi hicho katika ‘Jackpot’
ya wiki hii katika droo ya kusisimua iliyoonyeshwa siku ya jumapili
kupitia vituo vya runinga kote nchini.
Bwana
Changadiko ambaye anafanya kazi kama fundi minara mjini Dodoma
alielezea furaha yake juu ya ushindi huo ambao hakuutegemea na
akaishukuru Tatumzuka kwa kutimiza hitaji lake la pesa wakati alipokuwa
akizihitaji zaidi.
"Niliamua
kucheza Tatu Mzuka kutokana na matatizo niliyokuwa nayo ya kifedha
ambapo nilihitaji fedha za haraka ili kukidhi mahitaji hayo. Kwakweli
nina furaha kubwa sana na nashukuru kwamba nilijaribu bahati na
ikatimia” alisema.Mavunde alimpongeza mshindi kwa kushinda kiasi hicho
na Tatu Mzuka kwa ajili ya kuendelea kutengeneza mamilionea na
kubadilisha maisha ya watu.

Naibu Waziri Kazi, Vijana na Ajira (kushoto) Mh. Antony Mavunde (Mbunge), akimkabidhi mshindi wa 14 wa mchezo wa tatu Mzuka Bw. Robert A. Changadiko(45), hundi ya shilingi milioni sitini , Mjini Dodoma.

Mshindi wa droo ya 14 ya Tatu Mzuka Bw.Robert A. Changadiko (kulia)aliyejishindia donge nono la shilingi milioni sitini wiki hii, akiwa na rafiki yake bwana Bw. Daudi Mwangoto (katikati), ambaye alizawadiwa shilingi milioni moja kutoka katika promosheni ya cheza na washkaji shinda na washkaji ya Tatu Mzuka, kushoto ni Bw.Edwin Kawito ni mshindi wa Tatu Mzuka droo ya kumi (10) aliyejishindia shilingi milioni sitini.

Mshindi wa shilingi milioni sitini kutoka kijiji cha Msembata (Dodoma)Bw.Robert A. Changadiko mwenye umri wa maika 45, ambaye ni fundi minara,akifurahia ushindi wake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...