Michoro
mitatu iliyochorwa na watoto kutoka Tanzania hivi karibuni ilitunukiwa
tuzo ya heshima ya vyeti vya stashahada ya maonesho na Taasisi ya Sanaa
za watoto na vijana ya Hyvinkää, Finland.
Bryton Manyewa(10), Neev Mistry (9) wa shule ya Academic International Primary na Mandela Mtaya (5) wa shule ya chekechea ya Upendo Montessori ndiyo waliofanikiwa kupata tuzo hiyo kwa upande wa Tanzania baada ya kushiriki shindano la michoro liloitwa 'Pamoja' lililotayarishwa na taasisi hiyo ya nchini Finland.
Bryton Manyewa(10), Neev Mistry (9) wa shule ya Academic International Primary na Mandela Mtaya (5) wa shule ya chekechea ya Upendo Montessori ndiyo waliofanikiwa kupata tuzo hiyo kwa upande wa Tanzania baada ya kushiriki shindano la michoro liloitwa 'Pamoja' lililotayarishwa na taasisi hiyo ya nchini Finland.
Zaidi
ya michoro 6800 toka katika nchi 66 duniani zilishiriki shindano hilo
ambapo majaji ambao walikuwa ni wachoraji magwiji a sanaa wa nchi hiyo
walichagua michoro 670 kushiriki katika maonesho yaliyoanza Oktoba mwaka
huu na yatamalizika 18 Januari 2018 kwenye ukumbi wa Taasisi hiyo
inayojihusisha na elimu ya Sanaa kwa watoto na vijana ukuzaji wa
muingiliano wa utamaduni wa nchi mbalimbali.
Maonesho hayo yanaweza pia kutazamwa katika mfumo wa Kidijitali kupitia tovuti ya Taasisi hiyo www.artcentre.fi
Katika miaka ya nyuma, kwa ufadhili wa ubalozi wa Finland nchini, baadhi ya watoto kutoka Tanzania waliweza kuhudhuria mafunzo ya Sanaa yanayotolewa na taasisi hiyo
Katika miaka ya nyuma, kwa ufadhili wa ubalozi wa Finland nchini, baadhi ya watoto kutoka Tanzania waliweza kuhudhuria mafunzo ya Sanaa yanayotolewa na taasisi hiyo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...