Mitambo ya kuzalisha umeme (System Turbine, no 2) kwa ajili ya mradi wa kutumia gesi asilia wa Kinyerezi II iliingia nchini kupitia Bandarini Oktoba 16, 2017 na leo hii Novemba 03, 2017 imetolewa Bandarini na hivi sasa inaelekea kituo cha kuzalisha umeme kwa gesi Kinyerezi II (MW 240) Jijini Dare es Salaam.
Mradi huu wa Kinyerezi II uliwekwa jiwe la msingi na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli achi 16, 2016. Mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 2018.
Moja ya Gari iliyobeba Mitambo ya kuzalisha umeme (System Turbine, no 2) kwa ajili ya mradi wa kutumia gesi asilia wa Kinyerezi II ikielekea eneo Kutakapojengwa Mradi huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...