Mkuu
wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amemuagiza Mkurugenzi wa Bodi ya
Korosho CBT Hassan Jarufu pamoja na Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika
MAMCU Kuhakikisha wanaandika Barua ya Kutoa Maelezo kwa nini
Waliidanganya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuhusiana na Mkataba, Idadi ya
Ununuzi wa Magunia ya Kubebea Korosho katika Kikao Kilichoketi
Novemba,mosi Mwaka huu.
Katika Kikao hicho Bodi ya Korosho Kupitia MAMCU walisema, wameagiza magunia Million1 kupitia Kampuni ya DIRMAN HOLDING LTD na Ndipo mkuu wa Mkoa akaagiza Kuletewa mkataba Huo na kubaini kuwa Baadhi ya wajumbe wa Mamcu Hawaujui Mkataba na Haujulikani Thamani yake laki pia Mkataba ni magunia Laki6.5 na sio Million1 walizozisema katika kikao Hicho.Hata hivyo magunia hayo mpaka sasa hayajulikani idadi kamili iliyoletwa
Katika Mkutano na waandishi wa Habari Ofini kwake, Mkuu wa mkoa Byakanwa amesema kutokana na Udanganyifu huo Ofisi yake imeamua Bodi ya Korosho isilipe Pesa yeyote kwa kampuni ya DIRMA HOLDING LTD kwa kushindwa kuleta magunia kwa wakati,kwani ilitakiwa kuleta Septemba 30/2017lakini mpaka sasa bado hajakamilisha na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya Mzabuni huyo.
Aidha Ameiagiza Bodi kuhakikisha inasambaza magunia ndani ya Kipindi cha Wiki Mbili zijazo ili malalamiko ya wakulima yaweze kuondoka.
Kutokana na Udanganyifu Huo Mkuu wa Mkoa anatarajia Kuunda kamati ili kuweza kuchunguza taratibu zinazotumika kuingia mikataba na wote waliohusika na kamati hiyo itaishauri nini cha kufanya kwa wahusika.
Katika Kikao hicho Bodi ya Korosho Kupitia MAMCU walisema, wameagiza magunia Million1 kupitia Kampuni ya DIRMAN HOLDING LTD na Ndipo mkuu wa Mkoa akaagiza Kuletewa mkataba Huo na kubaini kuwa Baadhi ya wajumbe wa Mamcu Hawaujui Mkataba na Haujulikani Thamani yake laki pia Mkataba ni magunia Laki6.5 na sio Million1 walizozisema katika kikao Hicho.Hata hivyo magunia hayo mpaka sasa hayajulikani idadi kamili iliyoletwa
Katika Mkutano na waandishi wa Habari Ofini kwake, Mkuu wa mkoa Byakanwa amesema kutokana na Udanganyifu huo Ofisi yake imeamua Bodi ya Korosho isilipe Pesa yeyote kwa kampuni ya DIRMA HOLDING LTD kwa kushindwa kuleta magunia kwa wakati,kwani ilitakiwa kuleta Septemba 30/2017lakini mpaka sasa bado hajakamilisha na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya Mzabuni huyo.
Aidha Ameiagiza Bodi kuhakikisha inasambaza magunia ndani ya Kipindi cha Wiki Mbili zijazo ili malalamiko ya wakulima yaweze kuondoka.
Kutokana na Udanganyifu Huo Mkuu wa Mkoa anatarajia Kuunda kamati ili kuweza kuchunguza taratibu zinazotumika kuingia mikataba na wote waliohusika na kamati hiyo itaishauri nini cha kufanya kwa wahusika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...