Serikali inatarajia kuzindua Ripoti ya Utafiti wa Kitaifa wa Matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2016/2017 katika Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani Desemba Mosi mwaka huu Jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Siku ya Maadhimisho ya UKIMWI Duniani.
"Hii ni ripoti muhimu sana inayotokana na utafiti ambao huwa unafanyika kila baada ya miaka minne, ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003/2004 ni taarifa ambayo husaidia kuonesha hali halisi ya maambukizi ya VVU kwa watu wa marika mbalimbali pamoja na mapendekezo ya kisera namipango ya kudhibiti UKIMWI nchini," amesema Mhe. Mhagama.
Aidha, amesema kuwa maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yenye kaulimbiu "Changia mfuko wa maisha, Tanzania bila Ukimwi inawezekana" yatatoa fursa ya kutathimini hali halisi na mwelekeo wa udhibiti UKIMWI Kitaifa na Kimataifa ikiwemo kutafakari changamoto, mafanikio na uimarishaji wa mikakati mbalimbali ya kudhibiti UKIMWI.
" Siku hii pia hutoa nafasi ya kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha yao kutokana na UKIMWI, kuwaenzi wale waliojitokeza na kutoa mchango wao katika kudhibiti UKIMWI, pamoja na kuwajali yatima waliotokana na vifo vinavyohusiana na ugonjwa wa UKIMWI" ameongeza Jenista Mhagama.
Pia amesema kuwa, lengo lingine ni kutafakari na kutekeleza kitaifa na kimataifa kauli mbiu inayotolewa kila mwaka kulingana na vipaumbele vya kidunia, kikanda na kitaifa.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Hayo yamesemwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Siku ya Maadhimisho ya UKIMWI Duniani.
"Hii ni ripoti muhimu sana inayotokana na utafiti ambao huwa unafanyika kila baada ya miaka minne, ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003/2004 ni taarifa ambayo husaidia kuonesha hali halisi ya maambukizi ya VVU kwa watu wa marika mbalimbali pamoja na mapendekezo ya kisera namipango ya kudhibiti UKIMWI nchini," amesema Mhe. Mhagama.
Aidha, amesema kuwa maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani yenye kaulimbiu "Changia mfuko wa maisha, Tanzania bila Ukimwi inawezekana" yatatoa fursa ya kutathimini hali halisi na mwelekeo wa udhibiti UKIMWI Kitaifa na Kimataifa ikiwemo kutafakari changamoto, mafanikio na uimarishaji wa mikakati mbalimbali ya kudhibiti UKIMWI.
" Siku hii pia hutoa nafasi ya kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha yao kutokana na UKIMWI, kuwaenzi wale waliojitokeza na kutoa mchango wao katika kudhibiti UKIMWI, pamoja na kuwajali yatima waliotokana na vifo vinavyohusiana na ugonjwa wa UKIMWI" ameongeza Jenista Mhagama.
Pia amesema kuwa, lengo lingine ni kutafakari na kutekeleza kitaifa na kimataifa kauli mbiu inayotolewa kila mwaka kulingana na vipaumbele vya kidunia, kikanda na kitaifa.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...