Serikali
imezindua mkakati unaolenga kutokomeza uvuvi haramu kwa kuanzisha operesheni ya
kutumia ndege maalumu itakayofanya doria katika eneo la bahari kuu.
Akizungumza
wakati wa kuzindua safari ya ndege ya kutoka nchini Mauritius iliyotua hapa
nchini, kwa mara ya kwanza kwa ajili ya kufanya doria ya majini, Naibu Waziri
wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega alisema lengo ni kudhibiti uvuvi
haramu katika eneo la bahari kuu.
Alisema
Serikali ya awamu ya tano imejipambanua juu ya ulinzi wa rasilimali za nchi,
ikiwamo meli ya uhakika ya majini, licha ya kukumbwa na dhoruba kubwa.
Amesema kutokana
na hali hiyo ndiyo maana wameunganisha nguvu kwa pamoja kati yao na Ukanda wa
nchi za Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi kudhibiti uvuvi haramu kwa njia
zote.“Tunaruhusu
ndege ya doria leo, ili kuongezea nguvu njia za kudhibiti wavuvi haramu,
tulianza kwa njia ya bahari na sasa ni kwa njia ya anga.
“Changamoto
ya uvuvi haramu ni kubwa, mtu anapiga bomu kwenye matumbawe anafanya uharibifu
ambao kuyatengeneza tena yanachukua zaidi ya miaka 100, huku yeye akiharibu kwa
dakika tano, ” alisema Ulega.
Ulega
alisema uharibifu huo ndiyo unachangia kuwatia umasikini wavuvi wengi kwa
sababu siyo rahisi kupata samaki karibuni na kulazimika kwenda mbali ambako
siyo rahisi kufika bila kuwa na vyombo maalumu.
Naibu
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya operesheni ya kutumia ndege
maalumu itakayofanya doria katika eneo la bahari kuu kudhibiti uvuvi
haramu, leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akishuka
kwenye ndege maalumu itakayofanya doria katika eneo la bahari kuu
kudhibiti uvuvi haramu mara baada ya kuikagua ndani.
Waziri
wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid
Mohamed na Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega
pamoja na viongozi mbalimbali wakiangalia ndege maalumu ya doria katika
eneo la bahari kuu kudhibiti uvuvi haramu.
Waziri
wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid
Mohamed naNaibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega na
viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja
Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega na Waziri wa
Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid
Mohamed akitoa zawadi kwa marubani wa ndege hiyo. Picha zote na Emmanuel
Massaka,Globu yajamii.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...