Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu sifa na taratibu za utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018. Taarifa hii inalenga kutoa ufafanuzi kufuatia maoni ya baadhi ya wadau kuwa baadhi ya waombaji mikopo wenye sifa wanakosa mikopo ya elimu ya juu.
i. Uyatima: Waombaji ambao wamefiwa na wazazi na hivyo kushindwa kumudu gharama za elimu ya juu. Kwa mwaka huu, waombaji yatima wanapaswa kuthibitisha uyatima wao kwa kuwasilisha vyeti vya vifo vya wazazi wao vilivyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA);
ii. Wenye ulemavu: Waombaji wa mikopo wenye ulemavu wanapaswa kuambatisha barua kutoka kwa Mganga Mkuu wa Wilaya au Mkoa inayothibitisha ulemavu huo;
iii. Uduni wa kipato: Waombaji ambao wanatoka kwenye familia zenye vipato duni, miongoni mwao wakiwamo wale wenye barua za uthibitisho kuwa waliosomeshwa kwenye masomo yao kabla ya kujiunga na elimu ya juu;



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...