Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) siku ya tarehe 03 Novemba, 2017 ilifanikiwa kumkamata Bwana Dunia Athumani Tema mkazi wa Buguruni, Dar es Salaam kwa tuhuma za kujifanya Mtumishi wa TRA na kutoa huduma kwa mteja ndani ya Ofisi ya TRA Kariakoo – Gerezani Jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kukamatwa mtuhumiwa huyo alifikishwa katika Kituo cha Polisi kilichopo Msimbazi, Dar es Salaam na kufunguliwa RB ya MS/RB/9263/17, KOSA: KUJIFANYA MTUMISHI WA UMMA (TRA).

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatoa wito kwa wananchi wote kutoa taarifa mara moja katika Vituo vya Polisi vilivyopo karibu, Ofisi za TRA zilizopo karibu au kupiga simu namba 0800780078 au 0800750075 endapo watakuwa na mashaka na mtu yeyote anaye wahudumia. Pia Mamlaka inawasisitiza wananchi wasikubali kupewa huduma zozote na mtu wanayemtilia mashaka.

TRA inapenda kuwakumbusha kwamba, watumishi wake wote wanapaswa kuvaa au kuwa na kitambulisho chenye majina na cheo wanapokuwa wanatimiza majukumu yao ya kila siku mahali popote.

‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’

Imetolewa na;
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Makao Makuu.
12/11/2017.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...