Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) siku ya tarehe 03 Novemba, 2017 ilifanikiwa
kumkamata Bwana Dunia Athumani Tema mkazi wa Buguruni, Dar es Salaam kwa
tuhuma za kujifanya Mtumishi wa TRA na kutoa huduma kwa mteja ndani ya
Ofisi ya TRA Kariakoo – Gerezani Jijini Dar es Salaam.
Mara baada
ya kukamatwa mtuhumiwa huyo alifikishwa katika Kituo cha Polisi
kilichopo Msimbazi, Dar es Salaam na kufunguliwa RB ya MS/RB/9263/17,
KOSA: KUJIFANYA MTUMISHI WA UMMA (TRA).
Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) inatoa wito kwa wananchi wote kutoa taarifa mara moja
katika Vituo vya Polisi vilivyopo karibu, Ofisi za TRA zilizopo karibu
au kupiga simu namba 0800780078 au 0800750075 endapo watakuwa na mashaka
na mtu yeyote anaye wahudumia. Pia Mamlaka inawasisitiza wananchi
wasikubali kupewa huduma zozote na mtu wanayemtilia mashaka.
TRA
inapenda kuwakumbusha kwamba, watumishi wake wote wanapaswa kuvaa au
kuwa na kitambulisho chenye majina na cheo wanapokuwa wanatimiza
majukumu yao ya kila siku mahali popote.
‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’
Imetolewa na;
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Makao Makuu.
12/11/2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...