Na Dotto Mwaibale
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila amewataka Vijana wasomi na wanataalumu nchini kumsaidia Rais Dk.John Magufuli kuliletea Taifa maendeleo.
Ndabila ametoa mwito huo jijini Dar es Salaam jana wakati akiwahutubia wasomi wanataaluma katika kongamano la siku moja la vijana wasomi kutoka makanisa mbalimbali ya kikristo lilifanyika Hoteli ya Landmark lenye lengo kwa wasomi hao kutumia taaluma walizonazo katika kuitumikia jamii na taifa kwa ujumla.
"Ninyi wasomi mmesomeshwa kwa ajili ya kuwatumia wananchi na taifa msaidieni Rais wetu John Magufuli kuliletea taifa la Tanzania na kanisa maendeleo kwani hakuna mtu mwingine tunaye mtegemea zaidi yenu" alisema Askofu Ndabila.
Askofu Ndabila aliwataka wasomi hao waende kwa wananchi wakawanoe na kuweza kuwiva kisawasawa ili waendenane na kasi ya maendeleo anayoihitaji Rais Magufuli.
Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Amina Sanga akitoa mada kwenye kongamano la siku moja la vijana wasomi kutoka makanisa mbalimbali ya kikristo lilifanyika Hoteli ya Landmark jijini Dar es Salaam jana lenye lengo wasomi hao kutumia taaluma walizonazo katika kuitumikia jamii na taifa kwa ujumla.
Kongamano likiendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...