

Waandishi wa habari wa Mkoa wa Kigoma kutoka vyombo mbalimbali wakiwa kwenye mafunzo ya siku mbili kuhusu kuripoti habari za wakimbizi na umakini dhidi ya changamoto ya uwepo wa sheria mpya ya habari mafunzo yaliyoandaliwa na shirika la umoja wa mataifa(UN)na kuratibiwa na MISATAN Tanzania.

Wawezeshaji wa mafunzo hayo kutoka kushoto ni Mhariri mtendaji wa Guardian Jesse Kwayu (kushoto)James Marenga Wakili kutoka mahakama kuu.

Afisa uhusiano na mawasiliano,Ofisi ya mratibu mkazi mashirika ya umoja wa mataifa(UN)Didi Nafisa akitoa mada kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)juu mradi wa pamoja wa Kigoma unaofanywa na mashirika 16 ya umoja wa mataifa katika kambi za wakimbizi zilizopo Mkoani humo.

Baadhi washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada kwa makini toka kwa mwezeshaji Jesse Kwayu(hayupo pichani).

Kaimu Mkurugenzi MISATAN Tanzania Gasirigwa Sengiyumva akisisitiza jambo kwa washiriki wa mafunzo hayo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...