Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa Kijinsia, Theodosia Mhulo kutoka WLAC Akifungua maadhimisho hayo katika ofisi za REDESO zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, ambapo alitoa wito kwa wana harakati na Wadau kwa ujumla kuanza kuwatumia Wanaume kama chachu ya mabadiliko katika vita ya ukatili wa Kijinsia nchini.
 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya REDESO, Abeid Kasazi akizungumza kabla ya kumakaribisha mgeni rasmi kufungua maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Duniani kote, yaliyofanyika katika ofisi za Taasisi hiyo zilizopo kinondoni Jijini Dar es Salaam.
 Mshauri kutoka  REDESO, Brigitha  Sedekia akitoa somo juu ya ukatili wa kijinsia  kwa watu waliofika katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
 Sehemu ya wageni waalikwa waliokuwa wamekaa Meza kuu wakati wa Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Duniani wakishiriki kuimba kwa pamoja
 Kundi la Muziki la Wakimbizi linalojulikana kwa jina la Bana ba Zambe wakitoa Burudani wakati wa Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Duniani
 Sehemu ya wageni waalikwa walioshiriki katika Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Duniani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...