KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited kupitia Gazeti la Michezo la Mwanaspoti, imekabidhi
zawadi za droo ya kwanza ya Promosheni ya Zali la Mwanaspoti ikiwa ni zawadi kwa wasomaji kuelekea
mwisho wa mwaka.
Zawadi hizo mbalimbali sita zikiwemo simu mbili(Smartphone), Tv mbili nchi 32 zikiwa na vinga’amuzi
vyake vya Azam huku zikiwa zimelipiwa mwzi mzima,Pikipiki moja na ticketi moja ya kwenda kushohudia
moja ya mechi kubwa nchini Wingereza.
Makabidhiano hayo yalifanyika Viwanja vya Taifa jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa Pikipiki, Joachim Gibson akikabidhiwa Kadi na Funguo wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi
za washindi wa droo ya kwanza ya Promosheni ya Zali la Mwanaspoti iliyofanyika Viwanja vya Taifa.
Meneja Masoko wa Mwananchi Communications Limited, Sarah Munema (kushoto) akimkabidhi
Aristides Alphonce, zawadi ya ticketi ya Uingereza mara baada ya kuibuka mshindi wa droo ya kwanza
ya Zali la Mwanaspoti katika hafla fupi iliyofanyika Viwanja vya Taifa jijini Dar es Salaam.
Meneja wa vipindi vya Michezo wa Azam TV, Baruani Mhuza(kulia) akimkabidhi Mkombozi Mubanga,
zawadi ya TV nchi 32 ikiwa na king’amuzi cha Azam TV kikiwa kimelipiwa mwezi mzima mshindi wa droo
ya kwanza ya Zali la Mwanaspoti katika hafla fupi iliyofanyika Viwanja vya Taifa jijini Dar es
Salaam.Kushoto ni Masoko wa Mwananchi Communications Limited, Sarah Munema.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...