
Na Karama Kenyuko-Globu ya Jamii.
Washtakiwa wamesomewa mashtaka yao na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga aliyekuwa akisaidiana na Pamela Shinyambala na Mwanaamina Kombakono.
Washtakiwa hao walitajwa kuwa ni, Kashinde Bundala, Said Ally, Mafunda Ali, Abdulrazak Baus, Mwamba Mungia, Hafidhi Said, Abubakari Nzige, Athumani Ngondo, Endrew Mlugu na Ahmed Magogo.
Mbele ya Hakimu Mwandamizi, Godfrey Mwambapa imedaiwa kati ya Oktoba Mosi na Novemba 3/2017 jijini Dar es Salaam mshtakiwa Bundala
chini ya kisingizio cha kuhudhuria mashindano ya Sankuku Judo na mafunzo aliajiri na kuwasafirisha watu tisa, Kwenda Milan nchini Italia kwa ajili ya kufanya kazi kwa nguvu.
Watu hao ni, Ally, Ali, Baus,Mungia Said, Nzige, Nyondo Mlugu na Magogo.
Katuga amedai Oktoba 5/ 2017 huko Mwananyamala, mshtakiwa Bundala alighushi barua ya Oktoba 5,2017 akionyesha kuwa Umoja Judo Klabu umeomba ushiriki wa timu ya Judo ya Tanzania katika mashindano ya 28 ya Sankuku Judo wakati akijua si kweli.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...