
Na Karama Kenyuko-Globu ya Jamii.
Washtakiwa wamesomewa mashtaka yao na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga  aliyekuwa akisaidiana na Pamela Shinyambala na Mwanaamina Kombakono.
Washtakiwa hao walitajwa kuwa ni, Kashinde Bundala, Said Ally, Mafunda Ali, Abdulrazak Baus, Mwamba Mungia, Hafidhi Said, Abubakari Nzige, Athumani Ngondo, Endrew Mlugu na Ahmed Magogo.
Mbele ya Hakimu Mwandamizi, Godfrey Mwambapa imedaiwa kati ya Oktoba Mosi na Novemba 3/2017 jijini Dar es Salaam mshtakiwa  Bundala 
chini ya kisingizio cha kuhudhuria mashindano ya Sankuku Judo na  mafunzo  aliajiri na kuwasafirisha  watu tisa, Kwenda Milan nchini Italia kwa ajili ya kufanya kazi kwa nguvu.
Watu hao ni,  Ally, Ali, Baus,Mungia Said, Nzige, Nyondo Mlugu na Magogo.
Katuga amedai Oktoba 5/ 2017 huko Mwananyamala, mshtakiwa Bundala alighushi barua ya Oktoba 5,2017 akionyesha  kuwa Umoja Judo Klabu  umeomba ushiriki  wa timu ya  Judo ya Tanzania  katika  mashindano ya 28  ya Sankuku Judo wakati akijua si kweli.


 
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...