Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati wamempokea rasmi Katibu Mkuu mpya, Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua, Makao Makuu ya Wizara, mjini Dodoma. Mapokezi hayo yalifanyika Oktoba 31, 2017 na kuongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Lusias Mwenda. Zifuatazo ni picha za matukio mbalimbali wakati wa mapokezi hayo.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu mpya wa Wizara, Dkt. Hamisi Mwinyimvua (kushoto), mara baada ya Katibu Mkuu kuwasili rasmi Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma.
Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua (kulia), akimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Lusias Mwenda (kushoto), mara baada ya kuwasili rasmi Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma.
Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua (kushoto), akisalimiana na wafanyakazi mbalimbali wa Wizara (kulia), alipowasili rasmi Makao Makuu ya Wizara, mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...